Ruka hadi kwenye maudhui makuu

DAWA YA KUTIBU FIGO

Dalili zamagonjwa ya figo hutofautiana kutoka mtu mmoja na mwingine. Hutegemea zaidi na ugonjwa uliopo na ukali wake. Mara nyingi dalili huwa za jumla na zisizodhihirika vyema, na kwa hivyo uchunguzi hukosewa na utambuzi wa ugonjwa haufanyiki mapema.

Dalili za kawaida za ugonjwa wa figo

  • Kuvimba uso
    Kuvimba uso, miguu na tumbo, ni ishara za ugonjwa wa figo. Dalili za kuvimba kutokana na ugonjwa wa figo huwa inaanzia chini ya kibukio cha jicho (eye lids) na hutambulika sana asubuhi. Kushindwa kwa figo ni sababu ya kawaida na muhimu ya kuvimba. Lakini tunahitaji kuelewa kuwa kuvimba si lazima iwe ni figo kushindwa. Kuna ugonjwa mwingine wa figo licha ya figo hufanya kuvimba kutokea (mfano nephritic syndrome). Hoja nyingine ni vema kuwekwa akilini ni kuwa kuvimba huenda kusionekane kabisa kwa wagonjwa wachache wa ugonjwa dhahiri wa figo kushindwa kazi.
  • Kukosa hamu ya chakula, kichefuchefu, na kutapika
    Kukosa hamu ya chakula, kusikia ladha isiyo ya kawaida mdomoni na kushindwa kula chakula vyema ni shida za kawaida zinazopatikana kwa watu wenye hitilafu ya figo. kushindwa kwa figo zaidi kwa sababu ya sumu nyingi mtu huwa na kichefuchefu, kutapika na kwikwi.
  • Kupanda kwa damu/ Shinikizzo la damu – hypertension
    Kwa wagonjwa wa kushidwa kwa figo kufanya kazi, shinikizo la damu ni kawaida. Iwapo shinikizo la damu kunatokea katika umri mdogo (chini ya miaka 30) au shinikizo la damu liko juu wakati wa uchunguzi, sababu yaweza kuwa shida ya figo.
Kuvimba kwa uso chini ya kibukio cha macho ya mara kwa mara inaonyesha dalili ya ugonjwa wa figo.
  • Anemia (ukosefu wa damu) na kuwa dhaifu
    Kuwa dhaifu, kuchoka mapema, kukosa kutulia sehemu ya kazi ni malalamishi ya mara kwa mara ya mtu mwenye anemia (low hemoglobin level). Wakati mwingine hizi ni dalili pekee za mtu mwenye hali za mwanzo za ugonjwa sugu wa figo kutofanya kazi. Iwapo anaemia haiponi baada ya matibabu kamili, ni vyema kufikiria kushindwa kwa figo kama moja ya sababu ya anemia hiyo.

  • Malalamishi yasiyo kawaida  
  • Kuumwa chini ya mgongo, kuumwa mwili, kujikuna na maumivu ya miguu (cramps) huwa ni malalamishi ya mara kwa mara ya ugonjwa wa figo. Kutoendelea kukuwa, mtu kuwa mfupi na kujikunja (bending) kwa mifupa ya miguu ni dalili nyingine kwa watoto wenye ugonjwa wa figo.

  • Malalamishi ya mkojo


    Dalili za kawaida za kulalamikia mkojo :
    1. 1. Kiwango cha mkojo kilichopungua, ambacho husababisha kuvimba ni wazi kwa magonjwa mbalimbali ya figo.
    2. 2. Muwasho wa mkojo, kukojoa mara kwa mara na kukojoa damu au usaha ni dalili za maambukizo ya njia ya mkojo.
    3. 3. Ugumu wa kukojoa kunaweza kusababisha ugumu wa kusukumwa na kupitisha mkojo, mkojo hafifu au kudondokwa kwa mkojo. Katika hali mbaya kabisa kutopitisha/ kuziba kabisa mkojo ni hali ya kawaida.
Ingawa mtu anaweza kuwa na dalili zilizotajwa hapo juu, hii haidhihirishi kuwa mtu huyu anaugua ugonjwa wa figo. Hata hivyo, kukiwa na dalili hizi, inahimizwa kumwona daktari na kuthibitisha kama kuna dalili yoyote ya ugonjwa wa figo kwa kupima na kufanya uchunguzi.
Ni vyema kukumbuka kuwa, shida kubwa za ugonjwa wa figo zinaweza kuwepo chini chini kwa muda mrefu bila dalili au ishara zozote muhimu.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

YOU HAVE A BRIGHT FUTURE. IF YOU WILL GIVE YOUR EARTHLY LIFE TO JESUS

https://mbochiherbal.blogspot.com But if you contract HIV you need to think through what you need to change in your life and then set to work to rebuild your immune system

WATU WA KALE WALIAMINI TANGAWIZI NI TIBA ZAIDI MAANA ILITIUBU MARADHI 28

WATU WAKALE WALITUMIA ZAO LA TANGAWIZI KAMA TIBA KWA KUTIBU TAKRIBANI MAGONJWA 28 NA 100% WALIPONA Tangawizi (kwa Kilatini zingiberis rhizoma; kwa Kiingereza: ginger) ni mzizi wa mtangawizi. Umbo la tangawizi ni kama lile la mzizi wa manjano na yote miwili hutumika kama viungo katika chakula. TANGAWIZI NI TIBA KUBWA IKITUMIWA VEMA Tangawizi huwa na utomvu wenye mafuta na kampaundi zinazofanya ukali wake. Utafiti wa kisasa umegundua tangawizi inaweza kusaidia katika matatizo ya utumbo na kuzuia kutapika Tangawizi inatazamiwa kupunguza maumivu ya viungo vilivyoathiriwa na rumatizimu na homa ya baridi yabisi (arthritis) KWENYE ELIMU YA KALE WALITUMIA TANGAWIZI KUJENGA AFYA Katika elimu ya tiba ya kale tangawizi ilitazamiwa kuwa na tabia nyingi za kujenga afya, lakini matokeo mengi yanayodaiwa mwilini hayajathibitishwa kisayansi: Imedaiwa kuwa na uwezo ufuatao wa kitiba: 1. kuondoa sumu mwilini Sumu ni dutu yoyote inayoweza kuharibu kiasi kidogo shughuli za seli au inayo...

TIBA YA SHINIKIZO LA JUU LA DAMU

Shinikizo la juu la damu Shinikizo la juu la damu (HTN) au presha ya juu ya damu (pia huitwa shinikizo la mishipa ya damu , HBP), ni ugonjwa sugu ambapo nguvu ya msukumo wa damu katika mishipa ni kubwa kuliko kawaida. Ongezeko hilo husababisha moyo kufanya kazi kupita kiasi ili uzungushe damu katika mishipa ya damu. Kwa kawaida halina dalili, ila likidumu lina madhara makubwa kwa afya. Shinikizo la juu la damu ndilo sababu kubwa (kihatarishi) ya upoozaji, mshtuko wa moyo (mashambulizi ya moyo), moyo kushindwa kufanya kazi, kutuna kwa ukuta wa mishipa (k.m., kutuna kwa ukuta wa aota au mkole), chujio la mshipa wa kupeleka damu kwenye moyo au peripheral arterial disease, na inasababishwa na ugonjwa sugu wa figo. Hata ongezeko la wastani la shinikizo la damu hupunguza matarajio ya muda wa kuishi. Kuna vipimo viwili vya shinikizo la damu, yaani systolic na diastolic: shinikizo au presha ya systolic ni kipimo cha damu ambacho kinapima nguvu ya msukumo wa damu katika mish...