Tatizo la kutoa harufu ukeni husababishwa na sababu kadhaa Kama ifuatavyo.
1.Bacterial vaginosis
Kwa kawaida, uke huwa na bakteria ambao huitwa lactobacilli, bakteria hawa ni wazuri na hawamletei shida yeyote mwanamke, bakteria hawa huulinda uke usishambuliwe na bakteria wabaya ambao ndio husababisha magonjwa. Kinachowawezesha bakteria hawa waweze kukaa kwenye uke ni hali ya utindikali wa uke(vaginal acidity); hali hii ya utindikali wa uke inapobadilika na kupungua kwa sababu yeyote ile, husababisha bakteria hawa kupungua, na hivyo kutoa nafasi kwa bakteria wabaya kukua kwa wingi, na kushambulia afya ya uke, hivyo kusababisha harufu(harufu hii hutokana na uchafu unaotengenezwa na bakteria hawa).Hali hii kitaalamu ndio huitwa bacterial vaginosis.Ni muhimu kufahamu kuwa ugonjwa huu hauambukizwi kwa njia ya zinaa, japokuwa wanawake ambao wanajihusisha katika ngono wanakuwa katika hatari kubwa zaidi ya kpata ugonjwa huu, pia wanwake wanaofanya “douching”(kujisafisha ukeni kwa kuingiza kidole) na wanaoshiriki mapenzi kinyume cha maumbile wako kwenye uwezekano mkubwa wa kupata bacterial vaginosis.
2.Magonjwa ya zinaa (Sexually transmitted diseases;Vaginal Trichomoniasis, gonorrhea,chlamydia)
Ugonjwa wa zinaa unaoitwa kitaalamu vaginal trichomoniasis ndio
ugonjwa wa zinaa ambao unaathiri wanawake wengi zaidi kuliko ugonjwa
mwingine wowote wa zinaa. Ugonjwa huu unasababishwa na protozoa
anaejulikana kwa jina la Trichomona vaginalis. Na huambukizwa kwa njia
ya ngono. Dalili za ugonjwa huu kwa wanawake ni kutoa majimaji yanayotoa
harufu kali, yenye rangi ya njano–kijani,kuwashwa ukeni.
Gonorrrhea kwa kawaida pia huweza kusababisha kutokwa na
majimaji yenye harufu ukeni, na kuwashwa, maumivu wakati wa kukojoa,
maumivu wakati wa kufanya mapenzi, na maumivu chini ya kitovu (japokuwa,
kwa gonorhea wanawake wengi wanaweza wasionyeshe dalili yoyote kwa muda
mrefu).
Mara nyingi, inaweza kuwa vigumu kwa daktari kuweza kutofautisha baina
ya magonjwa haya ya zinaa (hasa kwa mazingira yetu duni); Hivyo basi
mara nyingi daktari atatoa dawa kwa ajili ya magonjwa haya matatu ya
zinaa pale anapofikiri kuwa mgonjwa wake ana tatizo la ugonjwa wa zinaa.
3.Fangasi za ukeni (Vagina candidiasis)
Fangasi za ukeni pia huweza kusababisha kutokwa na harufu kali ukeni,
japokuwa si kwa kiwango kikubwa sana kama sababu mbili hapo juu. Pia,
mara nyingi mwanamke mwenye tatizo la fangasi za ukeni atalalamika
kuhusu kuwashwa zaidi kuliko harufu.
Dalili za fangasi za ukeni ni pamoja na kutoa majimaji mazito ya rangi
nyeupe (kama maziwa mtindi) yenye harufu, kuwashwa ukeni,pamoja na
kusikia maumivu wakati wa kufanya mapenzi.
Vitu ambavyo vinamuweka mwanamke katika hatari ya kupata fangasi za
ukeni ni pamoja na kufanya “douching” (kujisafisha uke kwa kuingiza
kidole), kuvaa nguo za kubana, kuvaa nguo za ndani ambazo sio za cotton,
kuvaa nguo za ndani ambazo hazijapigwa na jua/kupigwa pasi, usafi
hafifu wa sehemu za siri, matumizi ya vyoo vya kukaa na matumizi ya dawa
za uzazi wa mpango.
Je, nini cha kufanya ili kujiepusha na harufu mbaya ya sehemu za siri kwa mdada?
-Epuka kusafisha uke kwa kuingiza kidole ukeni-Uke usafishwe kwa maji ya vuguvugu na sabuni ya kawaida ya kuogea (sio medicated soap), bila kuingiza kidole au kitu chochote ndani ya uke
-Epuka matumizi ya madawa ya antibiotics kwa muda mrefu bila ya
kuambiwa na daktari-kwani dawa hizi zikitumika kwa muda mrefu na bila
ushauri wa daktari husababisha mabadiliko katika bakteria wa kwenye uke
na kupelekea magonjwa na harufu mbaya
-Vaa nguo za ndani za cotton
-Epuka nguo za kubana sana mwili
-Nguo ya ndani ianikwe nje; sehemu ambayo itapigwa na jua (na sio ndani
ya chumba); au nguo za ndani zipigwe pasi kabla ya kuvaliwa,
-Unapokuwa kwenye siku zako zingatia usafi na kubadilisha pedi kama inavyotakiwa(mara 2-3 kwa siku)
-Epuka kutumia vyoo vya umma ambavyo ni vya kukaa,
-Jikinge na magonjwa ya zinaa,
-Epuka kuvaa nguo nyingi na/au nzito wakati wa kulala; vaa nguo nyepesi ambayo itaruhusu uke kupata hewa ya kutosha.
-Jisafishe vizuri kila baada ya kumaliza haja ndogo,
-Kitu kingine ambacho ni muhimu sana kufahamu, ikitokea ukaona kuwa uke
wako unatoa harufu, kuuosha kwa maji mengi na sabuni nyingi mara nyingi,
sio suluhisho bali unazidi kuleta matatizo zaidi kwa sababu unazidi
kupunguza idadi ya bakteria wazuri, na kubadilisha hali ya utindikali wa
uke na hivyo kukaribisha bakteria wabaya kwa wingi zaidi!!
-Na kitu cha mwisho ambacho ni muhimu zaidi, ni kwetu wanaume, unapoona
mwenzi wako ana tatizo hili, usimseme vibaya au kumkaripia au kumtukana;
Unatakiwa kutambua kuwa huo ni ugonjwa na umsaidie kuweza kuonana na
wataalamu wa tiba kwa ajili ya matibabu.
Maoni